Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 150:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Msifuni kwa mlio wa tarumbeta; msifuni kwa zeze na kinubi!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Msifuni kwa mlio wa tarumbeta; msifuni kwa zeze na kinubi!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Msifuni kwa mlio wa tarumbeta; msifuni kwa zeze na kinubi!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,

Tazama sura Nakili




Zaburi 150:3
17 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la BWANA kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.


Daudi na nyumba yote ya Israeli wakacheza mbele za BWANA kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa kayamba, na kwa matoazi.


na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya sauti ya Alamothi;


Na Shebania, na Yoshafati, na Nethaneli, na Amasai, na Zekaria, na Benaya, na Eliezeri, makuhani, wakapiga baragumu mbele ya sanduku la Mungu; na Obed-edomu na Yehia walikuwa mabawabu kwa ajili ya sanduku.


Ndivyo Israeli wote walivyolipandisha sanduku la Agano la BWANA kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga sauti kuu kwa vinanda na vinubi.


na pamoja nao Hemani na Yeduthuni wenye baragumu na matoazi, kwa hao watakaovumisha sauti, na vinanda kwa ajili ya hizo nyimbo za Mungu; na hao wana wa Yeduthuni wawepo mlangoni.


Tena Daudi na makamanda wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi kulingana na utumishi wao;


Wakafika Yerusalemu wenye vinanda, vinubi na parapanda kwenda nyumbani kwa BWANA.


hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru BWANA nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu BWANA, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya BWANA,


Amka, kinanda na kinubi, Nitaamka alfajiri.


Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.


Mshukuruni BWANA kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.


Kwa chombo chenye nyuzi kumi, Na kwa kinanda, Na kwa mlio wa kinubi.


wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zumari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha.


Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo