Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 147:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Bwana wetu ni mkuu, ana nguvu nyingi; maarifa yake hayana kipimo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Bwana wetu ni mkuu, ana nguvu nyingi; maarifa yake hayana kipimo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Bwana wetu ni mkuu, ana nguvu nyingi; maarifa yake hayana kipimo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.

Tazama sura Nakili




Zaburi 147:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana; Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.


Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu yeyote; Ana uweza katika nguvu za fahamu.


Maana najua ya kuwa BWANA ni mkuu, Na Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.


BWANA ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hauchunguziki.


Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.


Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu.


Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.


BWANA ni mkuu katika Sayuni, Naye ametukuka juu ya mataifa yote.


Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.


Hapana hata mmoja aliye kama wewe, Ee BWANA; wewe ndiwe uliye mkuu, na jina lako ni kuu katika uweza.


Ni nani asiyekucha wewe, Ee mfalme wa mataifa? Maana hii ni sifa yako wewe; kwa kuwa miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa, na katika hali yao ya enzi yote pia, hapana hata mmoja kama wewe.


Danieli akajibu, akasema, Na lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na uweza ni wake.


BWANA si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; BWANA ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.


Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!


Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo