Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 147:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Maana amevikaza vipingo vya malango yako, Amewabariki wanao ndani yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Maana yeye huimarisha milango yako, huwabariki watu waliomo ndani yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Maana yeye huimarisha milango yako, huwabariki watu waliomo ndani yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Maana yeye huimarisha milango yako, huwabariki watu waliomo ndani yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 147:13
20 Marejeleo ya Msalaba  

Makuhani na Walawi wakajitakasa, nao wakawatakasa watu, na malango, na ukuta.


Basi ikawa, walipoarifiwa Sanbalati, na Tobia, na Geshemu, Mwarabu na adui zetu hao wengine, kwamba nimeujenga ukuta, wala hayakubakia mapengo ndani yake; (ijapokuwa hata wakati ule sijaisimamisha milango katika malango);


Ikawa, baada ya ukuta kujengwa, na milango kuisimamishwa na kuweka mabawabu, waimbaji na Walawi,


Nikawaambia, Yasifunguliwe malango ya Yerusalemu kabla jua halijachomoza; na kabla walinzi hawajaondoka waifunge milango, mkaikaze; kisha wekeni walinzi wa zamu wa hao wakaao Yerusalemu, kila mtu na zamu yake, na kila mtu kuielekea nyumba yake.


Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo BWANA anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele.


Wavulana wetu wakiwa ujanani wawe kama miche Iliyostawi kikamilifu. Binti zetu wawe kama nguzo za pembeni Zilizochongwa ili kupamba kasri.


Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, Uzijenge kuta za Yerusalemu.


BWANA asema hivi, katika mahali hapo ambapo mnasema kwamba ni ukiwa, hapana mwanadamu wala mnyama, naam, katika miji ya Yuda na katika njia za Yerusalemu, zilizo ukiwa, hazina mwanadamu wala mwenyeji wala mnyama,


itasikika tena sauti ya furaha na sauti ya shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti yao wasemao Mshukuruni BWANA wa majeshi, maana BWANA ni mwema, rehema zake ni za milele; na sauti zao waletao sadaka za shukrani nyumbani kwa BWANA. Kwa kuwa nitawarudisha wafungwa wa nchi hii kama kwanza, asema BWANA.


Wafalme wa dunia hawakusadiki, Wala wote wakaao duniani, Ya kwamba mtesi na adui wangeingia Katika malango ya Yerusalemu.


Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo