Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 142:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Unitoe humu kifungoni, ili nipate kukushukuru. Watu waadilifu watajiunga nami kwa sababu umenitendea mema mengi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Unitoe humu kifungoni, ili nipate kukushukuru. Watu waadilifu watajiunga nami kwa sababu umenitendea mema mengi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Unitoe humu kifungoni, ili nipate kukushukuru. Watu waadilifu watajiunga nami kwa sababu umenitendea mema mengi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 142:7
20 Marejeleo ya Msalaba  

Ee nafsi yangu, urudi pumzikoni mwako, Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.


Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.


Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelitumainia neno lako.


Naam, nitamwimbia BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.


Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA, Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.


Ee BWANA, uniponye kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;


Ee BWANA, uniponye kutoka kwa adui zangu; Nimekukimbilia Wewe, unifiche.


Huwafanyia hukumu walioonewa, Huwapa wenye njaa chakula; BWANA hufungua waliofungwa;


Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha mahali penye usalama.


Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie na kufurahi.


Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nilifuata lililo jema.


Ili nizisimulie sifa zako zote; Katika malango ya binti Sayuni Nitaufurahia wokovu wako.


Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia mbele zako.


Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubirie wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwatibu waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.


ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.


Angalieni, twawaita heri wao waliostahimili. Mmesikia habari za kustahimili kwake Ayubu, kuona mwisho Bwana aliyomtendea, jinsi Bwana alivyo mwingi wa rehema na mwenye huruma.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo