Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 140:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Hao wanaonizingira wanainua vichwa; uovu wa maneno yao uwapate wao wenyewe!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Hao wanaonizingira wanainua vichwa; uovu wa maneno yao uwapate wao wenyewe!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Hao wanaonizingira wanainua vichwa; uovu wa maneno yao uwapate wao wenyewe!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zilizosababishwa na midomo yao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.

Tazama sura Nakili




Zaburi 140:9
11 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Zereshi mkewe na marafiki wote wa Hamani wakamwambia, Na kitengenezwe kiunzi cha mti wa kunyongea wa urefu wa mikono hamsini, na kesho asubuhi useme na mfalme ili Mordekai atundikwe juu yake; ndipo utakapoingia kwa furaha pamoja na mfalme karamuni. Basi ushauri huu ukamridhisha Hamani, akautengeneza mti wa kunyongea.


Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


Kwa ajili ya ulimi wao wataangamizwa; Wote wawaonao watatetemeka kwa hofu. Wote wawaonao watatikisa kichwa.


Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.


Naye atawarudishia uovu wao, Atawaangamiza katika ubaya wao, Naam, BWANA, Mungu wetu, atawaangamiza.


Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,


Baraka humkalia mwenye haki kichwani; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.


Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu.


Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.


Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.


Isipokuwa niliogopa makamio ya adui, Adui zao wasije wakafikiri uongo, Wasije wakasema, Mkono wetu umetukuka, Wala BWANA hakuyafanya haya yote.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo