Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:96 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

96 Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali amri yako haina kikomo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

96 Nimetambua kila kitu hufikia kikomo, lakini amri yako ni kamilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

96 Nimetambua kila kitu hufikia kikomo, lakini amri yako ni kamilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

96 Nimetambua kila kitu hufikia kikomo, lakini amri yako ni kamilifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

96 Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mwisho.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

96 Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:96
23 Marejeleo ya Msalaba  

Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hadi utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake.


Na ushauri wake Ahithofeli, aliokuwa akiutoa siku zile, ulikuwa kama mtu aulizapo kwa neno la Mungu; ndivyo yalivyokuwa mashauri yote ya Ahithofeli, kwa Daudi, na kwa Absalomu.


Naye Ahithofeli alipoona ya kuwa ushauri wake haukufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka, akaenda nyumbani kwake, mjini mwake, akaitengeneza nyumba yake, akajinyonga; akafa, akazikwa kaburini mwa babaye.


Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua mikuki mitatu midogo mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa bado hai katikati ya ule mwaloni.


Nao wakamtwaa Absalomu wakamtupa katika shimo kubwa mle msituni, wakaweka juu yake rundo kubwa sana la mawe; kisha Israeli wote wakakimbia kila mtu hemani mwake.


Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!


Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kufukuza upepo, wala faida hakuna chini ya jua.


Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, atendaye mema pasipo kutenda dhambi.


Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.


Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.


lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.


Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.


Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi.


Naye alikuwa na mwana, aliyeitwa Sauli, kijana, tena mzuri; wala katika wana wa Israeli hakuwako mtu mzuri kuliko yeye; tangu mabega yake kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wote.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo