Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:53 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

53 Ghadhabu kuu imenishika kwa sababu ya wasio haki, Waiachao sheria yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

53 Nashikwa na hasira kali, nionapo waovu wakivunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

53 Nashikwa na hasira kali, nionapo waovu wakivunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

53 Nashikwa na hasira kali, nionapo waovu wakivunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

53 Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

53 Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:53
15 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu, akaingia katika chumba cha Yehohanani, mwana wa Eliashibu; hata, alipofika huko, hakula mkate, wala hakunywa maji; kwa maana alilia kwa sababu ya kosa lile la watu wa uhamisho.


je! Tuzivunje tena amri zako, tukajiunge na watu wanaotenda machukizo hayo, kwa kuoana nao? Je! Usingekasirika nasi hata kutuangamiza kabisa, pasisalie mabaki yoyote, wala mtu wa kuokoka?


Nami niliposikia hayo, nikararua nguo yangu na joho langu, nikang'oa nywele za kichwa changu, na ndevu zangu, nikaketi kwa mshangao.


Nikagombana nao, nikawalaani, nikawapiga baadhi yao, na kuwang'oa nywele zao; nikawaapisha kwa Mungu, nikasema, Msiwaoze wana wao binti zenu, wala msiwatwae binti zao ili waolewe na wana wenu, wala na ninyi wenyewe.


Nami nilikasirika sana, niliposikia kilio chao, na maneno hayo.


Macho yangu yachuruzika mito ya machozi, Kwa sababu hawaitii sheria yako.


Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako.


Wanawe wakiiacha sheria yangu, Wasiende katika hukumu zangu,


Bali kama hamtaki kusikia, roho yangu italia kwa siri, kwa sababu ya kiburi chenu; na jicho langu litalia sana na kutoka machozi mengi, kwa kuwa kundi la BWANA limechukuliwa mateka.


Ndipo Danieli, aliyeitwa jina lake Belteshaza, akashangaa kwa muda, na fikira zake zikamfadhaisha. Mfalme akajibu akasema, Ee Belteshaza, ndoto ile isikufadhaishe wala tafsiri yake. Belteshaza akajibu, akasema, Bwana wangu, ndoto hii iwapate wao wakuchukiao, na tafsiri yake iwapate adui zako.


Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.


nami nitakapokuja tena, Mungu wangu asije akanidhili kwenu, nami nikawasikitikia wengi waliokosa tangu hapo, wasiutubie uchafu, na uasherati, na uovu walioufanya.


Maana wengi huenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo