Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:43 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

43 Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

43 Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

43 Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

43 Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

43 Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

43 Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:43
19 Marejeleo ya Msalaba  

Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.


Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe, Nami ninaziogopa hukumu zako.


Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.


Naamka kabla ya mapambazuko na kukuomba msaada, Naweka tumaini langu katika maneno yako.


Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu, Na hukumu zako zinisaidie.


Ninapozikumbuka hukumu zako za tangu kale, Ee BWANA, ninafarijika.


Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelitumainia neno lako.


Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelitumainia neno lako.


Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.


Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako?


BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.


Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.


Tena kuhusu habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.


Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, Habari Njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa mhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.


Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.


Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo