Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:26 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

26 Nilizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

26 Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu; unifundishe masharti yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

26 Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu; unifundishe masharti yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

26 Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu; unifundishe masharti yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

26 Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

26 Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:26
15 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya BWANA Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.


basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua katika nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao.


Nakusihi, BWANA, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.


Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, BWANA, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa BWANA.


Nimeapa nami nikathibitisha, Kuzishika hukumu zako za haki.


Ee BWANA, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.


Ee BWANA, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,


Ee BWANA, unifundishe njia yako, Na kuniongoza katika njia iliyonyoka; Kwa sababu yao wanaoniotea;


Ndipo nikakuungamia dhambi yangu, Wala sikuuficha upotovu wangu. Nilisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA, Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.


Kwa maana nitaungama uovu wangu, Na kusikitika kwa dhambi zangu.


Ee BWANA, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;


Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo