Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu, ambao wanakiuka amri zako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu, ambao wanakiuka amri zako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu, ambao wanakiuka amri zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa, wanaoenda mbali na amri zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:21
29 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini wao na baba zetu wakatakabari, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wala hawakuzisikiliza amri zako,


ukawashuhudia ili uwarudishe tena katika sheria yako; lakini walitakabari, wasizisikilize amri zako, bali wakayaasi maagizo yako, (ambazo mtu akizitenda ataishi katika hizo), nao wakayaondoa mabega yao, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wasitake kusikiliza.


Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.


Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sitoki katika njia ya mausia yako.


Umewakataa wote wazikosao amri zako, Kwa maana hila zao ni bure.


Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.


Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie.


Sasa najua ya kuwa BWANA ni mkuu kuliko miungu yote; naam, katika jambo hilo walilowatenda kwa ujeuri.


Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitamwadhibu matunda ya kiburi cha moyo wake mfalme wa Ashuru, na majivuno ya macho yake.


Ni nani aliyemtoa Yakobo awe mateka, aliyemtia Israeli katika mikono ya wanyang'anyi? Si yeye, BWANA? Yeye tuliyemkosea, ambaye hawakutaka kwenda katika njia zake, wala hawakuitii sheria yake.


Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa patakatifu, nami nitamfanya Yakobo kuwalaani, na Israeli kuwa tukano.


Neno lile ulilotuambia kwa jina la BWANA, sisi hatutakusikiliza.


Basi mimi, Nebukadneza, namhimidi Mfalme wa mbinguni, namtukuza na kumheshimu; maana matendo yake yote ni kweli, na njia zake ni za adili; na wale waendao kwa kutakabari, yeye aweza kuwadhili.


Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuri; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;


Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.


Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo