Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

18 Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Uyafumbue macho yangu, niyaone maajabu ya sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Uyafumbue macho yangu, niyaone maajabu ya sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Uyafumbue macho yangu, niyaone maajabu ya sheria yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:18
17 Marejeleo ya Msalaba  

Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali amri yako haina kikomo.


Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho kitabu, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza.


Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.


Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.


Nijapomwandikia sheria yangu katika amri makumi elfu, zimehesabiwa kuwa ni kitu kigeni.


Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.


Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Baryona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.


Wakamwambia, Bwana, twataka macho yetu yafumbuliwe.


Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.


uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.


Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wowote kuwakamilisha wakaribiao.


watumikiao mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema; maana asema, Angalia ukavifanye vitu vyote kwa mfano ule uliooneshwa katika mlima.


Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo