Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:165 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

165 Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

165 Wapendao sheria yako wana amani kuu; hakuna kinachoweza kuwaangusha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

165 Wapendao sheria yako wana amani kuu; hakuna kinachoweza kuwaangusha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

165 Wapendao sheria yako wana amani kuu; hakuna kinachoweza kuwaangusha.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

165 Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

165 Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:165
18 Marejeleo ya Msalaba  

Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.


Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.


Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa.


Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.


Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.


Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.


Naye atasema, Tutieni, tutieni, Itengenezeni njia, Ondoeni kila kizuizi Katika njia ya watu wangu.


Hapana amani kwa waovu; asema Mungu wangu.


lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa.


Kwa maana watatokea Makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, ikiwezekana, hata walio wateule.


Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.


Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.


Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala ndani yake hamna kikwazo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo