Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:161 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

161 Wakuu wameniudhi bure, Ila moyo wangu unakaa kwa kicho cha maneno yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

161 Wakuu wanidhulumu bila kisa, lakini mimi naheshimu maneno yako kwa moyo wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

161 Wakuu wanidhulumu bila kisa, lakini mimi naheshimu maneno yako kwa moyo wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

161 Wakuu wanidhulumu bila kisa, lakini mimi naheshimu maneno yako kwa moyo wote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

161 Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

161 Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:161
14 Marejeleo ya Msalaba  

Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu chochote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nimkosee Mungu?


Siku ya tatu, Yusufu akawaambia, Fanyeni hivi, mkaishi, maana mimi namcha Mungu.


kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekeza mbele za BWANA, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema BWANA.


Lakini watawala wa kwanza walionitangulia, wakawalemea watu, wakawatwalia chakula na mvinyo, zaidi ya shekeli arubaini za fedha; tena hata watumishi wao nao wakawatawala watu; lakini mimi sikufanya hivyo, kwa kuwa nilimcha Mungu.


Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu, Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.


Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini mimi sikiuki shuhuda zako.


Wakuu nao waliketi wakaninena, Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.


Muwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.


Je! Mimi nina haja ya watu wenye wazimu, hata mmemleta kiumbe huyu ili aoneshe wazimu wake machoni pangu? Je! Huyu ataingia nyumbani mwangu?


Akasema, Bwana wangu ananiwinda mimi mtumishi wake kwa sababu gani? Nimefanya nini mimi? Ni uovu gani nilio nao mkononi mwangu?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo