Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:126 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

126 Wakati umewadia BWANA atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

126 Ee Mwenyezi-Mungu, sasa ni wakati wa kufanya kitu, kwa maana watu wanavunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

126 Ee Mwenyezi-Mungu, sasa ni wakati wa kufanya kitu, kwa maana watu wanavunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

126 Ee Mwenyezi-Mungu, sasa ni wakati wa kufanya kitu, kwa maana watu wanavunja sheria yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

126 Ee Mwenyezi Mungu, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

126 Ee bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:126
14 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.


Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya BWANA Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.


Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.


Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, Na kuyaonea huruma mavumbi yake.


Inuka, ee BWANA, mwanadamu asipate nguvu, Mataifa wahukumiwe mbele zako.


Siku nyingi nimenyamaza kimya; nimenyamaza, nikajizuia; sasa nitapiga kelele kama mwanamke aliye katika kuzaa; nitaugua na kutweta pamoja.


Mwasemaje, Sisi tuna akili, na Torati ya BWANA tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Kwa sababu hiyo sheria imelegea, wala hukumu haipatikani; kwa maana watu wabaya huwazunguka wenye haki; kwa sababu hiyo hukumu inayotolewa huwa imepotoshwa.


Bali ninyi mmegeuka mkaiacha njia; mmewakwaza watu wengi katika sheria; mmeliharibu agano la Lawi, asema BWANA wa majeshi.


basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.


Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? La hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.


Maana ikiwa wale wa sheria ndio warithi, imani imekuwa bure, na ahadi imebatilika.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo