Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 119:116 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

116 Unitegemeze kulingana na ahadi yako, nikaishi, Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

116 Uniimarishe ulivyoahidi, nami nitaishi; usikubali niaibike katika tumaini langu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

116 Uniimarishe ulivyoahidi, nami nitaishi; usikubali niaibike katika tumaini langu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

116 Uniimarishe ulivyoahidi, nami nitaishi; usikubali niaibike katika tumaini langu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

116 Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

116 Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.

Tazama sura Nakili




Zaburi 119:116
16 Marejeleo ya Msalaba  

Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.


Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.


Ee Mungu wangu, Nimekutumainia Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.


Maana mikono ya wasio haki itavunjika, Bali BWANA huwategemeza wenye haki.


Ajapojikwaa hataanguka chini, Maana BWANA humshika mkono na kumtegemeza.


Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza, Umeniweka mbele za uso wako milele.


Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia; Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu.


Nafsi yangu inaambatana nawe sana; Mkono wako wa kulia unanitegemeza.


Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee BWANA, fadhili zako zilinitegemeza.


usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kulia wa haki yangu.


Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu.


Bali Israeli wataokolewa na BWANA kwa wokovu wa milele; ninyi hamtatahayarika, wala kufadhaika, milele na milele.


Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.


na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.


Kwa kuwa imeandikwa katika Maandiko: Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo