Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 106:45 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

45 Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

45 kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

45 kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

45 kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 106:45
22 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini huyo malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili auharibu, BWANA akaghairi katika mabaya, akamwambia huyo malaika mwenye kuwaharibu watu, Yatosha, sasa ulegeze mkono wako. Naye yule malaika wa BWANA alikuwako karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.


Lakini BWANA akawahurumia, akawasikitikia, na kuwaangalia, kwa ajili ya agano lake na Abrahamu, na Isaka, na Yakobo, wala hakutaka kuwaangamiza, wala hakuwatupa usoni pake bado.


Analikumbuka agano lake milele; Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Na kuwahurumia watumishi wake.


Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Ee Mungu, unirehemu, kulingana na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.


Ee BWANA, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee.


Urudi, Ee BWANA utakasirika hadi lini? Wahurumie watumishi wako.


Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.


Nitautaja wema wa BWANA, sifa za BWANA kwa yote aliyotukirimia BWANA; na wingi wa wema wake kwa nyumba ya Israeli, aliowakirimia kwa rehema zake, na kwa wingi wa wema wake.


ikiwa taifa lile nililolitaja litageuka, na kuacha maovu yake nitaghairi, nisitende mabaya yale niliyoazimia kuwatenda.


Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.


Walakini nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe, katika siku za ujana wako, nami nitaweka imara agano la milele pamoja nawe.


Niwezeje kukuacha, Efraimu? Niwezeje kukuachilia Israeli? Niwezeje kukufanya kama Adma? Niwezeje kukuweka kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zimewaka pamoja.


lakini kwa ajili yao nitalikumbuka agano la baba zao, niliowaleta watoke katika nchi ya Misri mbele ya macho ya mataifa, ili kwamba niwe Mungu wao; mimi ndimi BWANA.


BWANA akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema BWANA.


BWANA akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,


Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia BWANA; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli.


Na kila wakati BWANA alipowainulia waamuzi, ndipo BWANA alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana BWANA alisikitishwa na kilio chao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo