Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 106:41 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

41 Akawatia mikononi mwa mataifa, Nao waliowachukia wakawatawala.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

41 Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa, hao wenye kuwachukia wakawatawala.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

41 Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa, hao wenye kuwachukia wakawatawala.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

41 Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa, hao wenye kuwachukia wakawatawala.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.

Tazama sura Nakili




Zaburi 106:41
16 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na tuanguke katika mkono wa BWANA; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.


Basi, tazama, kwa ajili ya hayo nimenyosha mkono wangu juu yako, nami nimelipunguza posho lako, na kukutoa kwa mapenzi yao wanaokuchukia, binti za Wafilisti, walioyaonea haya mambo yako ya uasherati.


BWANA atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huku na huko katika falme zote za duniani.


utakwenda kwa kupapasapapasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.


Matunda ya nchi yako, na taabu yako yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na kupondwa chini daima;


kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta BWANA juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.


Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama BWANA asingaliwatoa?


Ndipo watu elfu tatu wa Yuda wakateremka hadi katika ule ufa wa jabali la Etamu, wakamwambia Samsoni, Je! Hujui ya kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hii, basi, uliyotutenda? Akawaambia, Kadiri ile walivyonitenda mimi, ndivyo nilivyowatenda wao.


Hasira ya BWANA ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao.


Basi wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu tena mbele za BWANA; naye BWANA akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu juu ya Israeli, kwa sababu walikuwa wameyafanya yaliyo maovu mbele za macho ya BWANA.


Wana wa Israeli walimtumikia Egloni mfalme wa Moabu muda wa miaka kumi na minane.


Kwa hiyo hasira za BWANA ziliwaka juu ya Israeli, naye akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia; na wana wa Israeli wakamtumikia huyo Kushan-rishathaimu muda wa miaka minane.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo