Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 105:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

16 Akasababisha njaa katika nchi, Akakiharibu chakula chote walichokitegemea.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Mungu alizusha njaa nchini mwao, akaharibu chakula chao chote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Mungu alizusha njaa nchini mwao, akaharibu chakula chao chote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Mungu alizusha njaa nchini mwao, akaharibu chakula chao chote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Akaiita njaa juu ya nchi na kuharibu chakula chao chote,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Akaiita njaa juu ya nchi na kuharibu chakula chao chote,

Tazama sura Nakili




Zaburi 105:16
17 Marejeleo ya Msalaba  

ikaanza kuja miaka ile saba ya njaa, kama vile Yusufu alivyosema. Kukawa na njaa katika nchi zote, bali katika nchi yote ya Misri palikuwa na chakula.


Baadaye hapakuwa na chakula katika nchi yote, kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana, hata nchi ya Misri na nchi ya Kanaani zikataabika, kwa sababu ya njaa.


Kwa nini tufe mbele ya macho yako, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu kwa chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao; kisha utupe mbegu, tuishi wala tusife, wala nchi yetu isipotee.


Basi Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke, ambaye alimfufulia mwanawe, akasema, Ondoka, ukaende wewe na jamaa yako, ukae hali ya kigeni utakakoweza kukaa; kwa sababu BWANA ameiita njaa; nayo itakuja juu ya nchi hii muda wa miaka saba.


Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Aung'aze uso wake kwa mafuta, Na mkate umburudishe mtu moyo wake.


Kwa maana, tazama, Bwana, BWANA wa majeshi, awaondolea Yerusalemu na Yuda egemeo na tegemeo; tegemeo lote la chakula na tegemeo lote la maji;


Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa hofu;


Hapo nitakapovunja tegemeo lenu la mkate, wanawake kumi wataoka mikate yenu katika tanuri moja, nao watawapa mikate yenu tena kwa kupima kwa mizani; nanyi mtakula, lakini hamtashiba.


Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta BWANA?


Niliwapiga kwa ukavu, na ukungu, na mvua ya mawe, katika kazi zote za mikono yenu; lakini hamkunirudia mimi, asema BWANA.


Basi kukawa na njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, na dhiki nyingi, wala baba zetu hawakupata chakula cha kuwatosha.


Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda jina lake ni Mauti, na Kuzimu akafuatana naye. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa wanyama wa nchi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo