Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 102:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Wewe utainuka na kuurehemu mji wa Siyoni; maana wakati umefika wa kuutendea mema; wakati wake uliopangwa umefika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Wewe utainuka na kuurehemu mji wa Siyoni; maana wakati umefika wa kuutendea mema; wakati wake uliopangwa umefika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Wewe utainuka na kuurehemu mji wa Siyoni; maana wakati umefika wa kuutendea mema; wakati wake uliopangwa umefika.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonesha wema; wakati uliokubalika umewadia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.

Tazama sura Nakili




Zaburi 102:13
26 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, jina lako linadumu milele, BWANA, sifa zako zitakumbukwa na vizazi vyote.


Uinuke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.


Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, Uzijenge kuta za Yerusalemu.


BWANA uondoke kwa hasira yako; Ujiinue Juu ya ujeuri wa watesi wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu.


Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.


Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia, Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.


Maana hao adui zako, Ee BWANA, Hao adui zako watapotea, Na watendao maovu watatawanyika wote pia.


Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, BWANA, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.


Wajumbe wa taifa hilo waletewe jibu gani? Ya kuwa BWANA ameiweka misingi ya Sayuni, na ndani yake wale walioonewa katika watu wake watapata kimbilio kwake.


Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa BWANA adhabu maradufu kwa dhambi zake zote.


Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa BWANA umekuzukia.


BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Watatumia tena neno hili katika nchi ya Yuda, na katika miji yake, nitakapowarudisha mateka yao; BWANA na akubariki, Ee makao ya haki, Ee mlima wa utakatifu.


Akasema, Nenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa mhuri, hata wakati wa mwisho.


Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.


Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,


mkiingojea hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?


Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo