Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 100:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Maana BWANA ni mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Mwenyezi-Mungu ni mwema; fadhili zake zadumu milele, na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Mwenyezi-Mungu ni mwema; fadhili zake zadumu milele, na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Mwenyezi-Mungu ni mwema; fadhili zake zadumu milele, na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Kwa maana Mwenyezi Mungu ni mwema na fadhili zake zadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Kwa maana bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.

Tazama sura Nakili




Zaburi 100:5
31 Marejeleo ya Msalaba  

Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru BWANA nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu BWANA, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya BWANA,


Wakaimbiana, wakimhimidi BWANA, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi BWANA, kwa sababu msingi wa nyumba ya BWANA umekwisha kuwekwa.


Bali fadhili za BWANA ni kwa wamchao Tangu milele hata milele, Na haki yake ni kwa vizazi vyote;


Haleluya. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.


Na wamshukuru BWANA, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.


BWANA atanitimizia malengo yake kwangu; Ee BWANA, fadhili zako ni za milele; Usiiache kazi ya mikono yako.


Aliyezifanya mbingu na nchi, Bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele,


BWANA yu mwema, mwenye adili, Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.


Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni, Uaminifu wako hadi mawinguni.


Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.


Fadhili na kweli zitakutana, Haki na amani zitakumbatiana.


Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao.


itasikika tena sauti ya furaha na sauti ya shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti yao wasemao Mshukuruni BWANA wa majeshi, maana BWANA ni mwema, rehema zake ni za milele; na sauti zao waletao sadaka za shukrani nyumbani kwa BWANA. Kwa kuwa nitawarudisha wafungwa wa nchi hii kama kwanza, asema BWANA.


Wewe utamtimilizia Yakobo kweli yako, na Abrahamu rehema zako, ulizowaapia baba zetu tangu siku za kale.


BWANA ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.


Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.


Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hadi vizazi elfu;


katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo