Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 9:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu, Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Yeye peke yake alizitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Yeye peke yake alizitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Yeye peke yake alizitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

Tazama sura Nakili




Yobu 9:8
22 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.


Maana miungu yote ya watu si kitu; Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.


Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake; Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.


Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.


Je! Waweza kuzitandaza mbingu pamoja naye, Ambazo zina nguvu kama kioo cha kuyeyushwa?


Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita, Na hapa mawimbi yako yenye nguvu yatazuiliwa?


Je! Umeziingia chemchemi za bahari, Au umetembea mahali pa siri pa vilindi?


Kwa neno la BWANA mbingu ziliumbwa, Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.


Njia yako ilikuwa katika bahari. Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; Hatua zako hazikujulikana.


Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;


Mungu BWANA anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.


BWANA, mkombozi wako, yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi; Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote; nizitandaye mbingu peke yangu; niienezaye nchi; ni nani aliye pamoja nami?


Ukamsahau BWANA, Muumba wako, yeye aliyezitanda mbingu, na kuiweka misingi ya dunia; nawe unaogopa daima mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu yake yeye aoneaye, hapo ajitayarishapo kuharibu; nayo i wapi ghadhabu yake aoneaye?


Mtawaambia hivi, Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu.


Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.


Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.


Ufunuo wa neno la BWANA juu ya Israeli. Haya ndiyo asemayo BWANA, azitandaye mbingu, auwekaye msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake.


Basi wakavuta makasia kadiri ya maili tatu nne, wakamwona Yesu anakwenda juu ya bahari na kuikaribia mashua; wakaogopa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo