Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 9:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Ingawa mimi ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; Ingawa mimi ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa mimi ni mpotovu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Ingawa sina hatia, maneno yangu yenyewe yangenihukumu; ingawa sina lawama, angenithibitisha kuwa mpotovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Ingawa sina hatia, maneno yangu yenyewe yangenihukumu; ingawa sina lawama, angenithibitisha kuwa mpotovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Ingawa sina hatia, maneno yangu yenyewe yangenihukumu; ingawa sina lawama, angenithibitisha kuwa mpotovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.

Tazama sura Nakili




Yobu 9:20
24 Marejeleo ya Msalaba  

Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


Mimi nikiwa mwovu, ole wangu! Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu; Maana nimejaa aibu Nikiyaangalia mateso yangu.


Kosa langu limetiwa mhuri mfukoni, Nawe waufunga uovu wangu.


Huyo Ayubu amesema pasipo maarifa, Na maneno yake hayana hekima.


Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa.


Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu? Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?


Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, siwezi kumjibu; Ni lazima nimwombe mshitaki wangu anihurumie.


Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?


Mimi ninayaogopa mateso yangu yote, Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.


Nitahukumiwa kuwa ni mkosa; Ya nini basi nitaabike bure?


BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?


Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.


Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.


Mtu mwenye moyo wa ukaidi hatapata mema; Na mwenye ulimi wa upotovu huanguka katika misiba.


Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, BWANA wa majeshi.


Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?


Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.


na kuzozana miongoni mwa watu waliopotoka katika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida.


Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo