Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 7:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 Nawe, je! Mbona hunisamehe makosa yangu, Na kuniondolea maovu yangu? Kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; Nawe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwapo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Mbona hunisamehi kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi punde nitalazwa chini kaburini, utanitafuta, lakini sitakuwapo tena!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Mbona hunisamehi kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi punde nitalazwa chini kaburini, utanitafuta, lakini sitakuwapo tena!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Mbona hunisamehi kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi punde nitalazwa chini kaburini, utanitafuta, lakini sitakuwapo tena!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”

Tazama sura Nakili




Yobu 7:21
29 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia BWANA, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee BWANA, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.


Nikifanya dhambi, ndipo waniangalia, Wala hutaniachilia na uovu wangu.


Kumbuka, nakusihi ulivyonifinyanga kama vile udongo; Nawe, je! Utanirudisha uvumbini tena?


Yuko nani atakayeshindana nami? Maana sasa nitanyamaza kimya na kukata roho.


Lakini mwanadamu hufa, hufariki dunia; Naam, mwanadamu hukata roho, naye yupo wapi?


Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na dada yangu;


Ataruka mfano wa ndoto, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,


Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho; Hufunua macho yake, naye hayuko.


Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;


Mimi ni safi, sina makosa; Sina hatia, wala hapana uovu ndani yangu;


Jicho lake huyo anionaye halitaniangalia tena; Macho yako yatanielekea, lakini sitakuwapo.


Ndipo Bildadi huyo Mshuhi akajibu, na kusema,


Mimi ninayaogopa mateso yangu yote, Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.


Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo anavyostawi.


Nikapita na kumbe! Hayuko, Nikamtafuta wala hakuonekana.


Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.


Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana umande wako ni kama umande wa mimea, nayo ardhi itawatoa waliokufa.


Ee BWANA, usione hasira nyingi, wala usiukumbuke uovu siku zote; tazama, angalia, twakusihi, sisi sote tu watu wako.


Tena, wengi wa hao wanaolala katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.


Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie BWANA; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng'ombe.


Kesho yake alimwona Yesu akija kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!


ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.


Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kututakasa na udhalimu wote.


Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo