Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 40:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 “Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu? Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 “Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu? Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 “Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu? Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

Tazama sura Nakili




Yobu 40:2
35 Marejeleo ya Msalaba  

Nitamwambia Mungu, Usinihukumie makosa; Nijulishe kwa nini unapingana nami.


Hakika ningenena naye huyo Mwenyezi, Nami nataka kuhojiana na Mungu.


Ningeiweka kesi yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja.


Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu; Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;


Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;


Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukigo?


Wewe umegeuka kuwa mkali kwangu; Nawe waniudhi kwa uweza wa mkono wako.


Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia! (Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu); Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!


Kwa nini unapingana naye, ukisema, Hatajibu hata neno langu moja?


Basi jifunge viuno kama mwanamume, Maana nitakuuliza neno, nawe niambie.


BWANA akafululiza kumjibu Ayubu, na kusema,


Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema,


Je! Mimi ni bahari, au je! Ni nyangumi? Hata ukawaweka walinzi juu yangu?


Kama akipenda kushindana naye, Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.


Na awe kitu chochote, aliitwa jina lake zamani za kale, naye amejulikana kuwa ndiye mwanadamu; wala hawezi kabisa kushindana na yeye aliye na uwezo kuliko yeye mwenyewe.


Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonesha njia ya fahamu?


Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye hasimu yangu? Na anikaribie basi.


Nimekutegea mtego, Ee Babeli, nawe ukanaswa, nawe ulikuwa huna habari; umeonekana, ukakamatwa, kwa sababu ulishindana na BWANA.


Je! Maana yake ni nini hata mkatumia mithali hii katika Israeli, mkisema, Baba wamekula zabibu mbichi, nao watoto wakatiwa ganzi la meno?


Basi wakiisha kuipokea, wakamnung'unikia mwenye nyumba,


Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?


Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo