Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 4:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Mungu huwaangamiza hao kwa pumzi yake, hao huteketezwa kwa pigo la hasira yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Mungu huwaangamiza hao kwa pumzi yake, hao huteketezwa kwa pigo la hasira yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Mungu huwaangamiza hao kwa pumzi yake, hao huteketezwa kwa pigo la hasira yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa; kwa mshindo wa hasira zake huangamia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa; kwa mshindo wa hasira zake huangamia.

Tazama sura Nakili




Yobu 4:9
13 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, nitatia roho ya hofu ndani yake, naye atasikia uvumi, na kuirudia nchi yake mwenyewe; nami nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.


mara, tazama, upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari.


Hataondoka gizani; Ndimi za moto zitayakausha matawi yake, Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.


Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhalilishe.


Wafiche mavumbini pamoja, Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.


Ndipo ilipoonekana mikondo ya maji, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Ee BWANA, kwa kukemea kwako, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwako.


Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu.


Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa kilima, Vilindi vikagandamana katikati ya bahari.


bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.


Maana Tofethi imewekwa tayari tokea zamani, naam, imewekwa tayari kwa mfalme huyo; ameifanya kubwa, inakwenda chini sana; tanuri yake ni moto na kuni nyingi; pumzi ya BWANA, kama mto wa kiberiti, huiwasha.


Majani yakauka, ua lanyauka; Kwa sababu pumzi ya BWANA yapita juu yake. Hakika watu ni majani.


Hapo ndipo atakapofunuliwa yule mwasi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa dhihirisho la kuja kwake;


Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo