Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 4:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 Je! Kamba ya hema yao haikung'olewa ndani yao? Nao hufa hata bila kuwa na hekima.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Iwapo uzi unaoshikilia uhai wao ukikatwa wao hufa tena bila kuwa na hekima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Iwapo uzi unaoshikilia uhai wao ukikatwa wao hufa tena bila kuwa na hekima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Iwapo uzi unaoshikilia uhai wao ukikatwa wao hufa tena bila kuwa na hekima.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Je, kamba za hema lao hazikung’olewa, hivyo hufa bila hekima?’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Je, kamba za hema yao hazikung’olewa, hivyo hufa bila hekima?’

Tazama sura Nakili




Yobu 4:21
15 Marejeleo ya Msalaba  

Hakika ndivyo yalivyo makazi ya wapotovu, Na hapa ni mahali pake asiyemjua Mungu.


Sio wakuu walio wenye hekima, Wala sio wazee watambuao haki.


Lakini wasiposikia, wataangamia kwa upanga, Nao watakufa pasipo maarifa.


Hao wakuchukiao watavikwa aibu; Nayo hema yake mwovu haitakuwako tena.


Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake, Watowesha uzuri wake kama nondo. Kila mwanadamu ni ubatili.


Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri; Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako. Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.


Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na kifo kitakuwa mchungaji wao; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Miili yao itaoza, kao lao ni kuzimu.


Mwanadamu mwenye heshima, iwapo hana akili, Amefanana na wanyama wapoteao.


Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.


Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;


Mwacheni mwanadamu ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake; kwa maana wanafaa kitu gani?


Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?


Maana jua huchomoza kwa joto kali, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo