Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 37:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Kwa kuwa huiambia theluji, Anguka juu ya nchi; Na pia kwa manyunyu ya mvua, Hayo manyunyu ya mvua yake nyingi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya nchi!’ Na manyunyu na mvua, ‘Nyesha kwa nguvu.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya nchi!’ Na manyunyu na mvua, ‘Nyesha kwa nguvu.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya nchi!’ na manyunyu na mvua, ‘Nyesha kwa nguvu.’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

Tazama sura Nakili




Yobu 37:6
14 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini watu hawa ni wengi, tena ni wakati wa mvua nyingi, nasi hatuwezi kusimama nje, tena kazi hii si kazi ya siku moja, wala ya siku mbili; maana tumekosa sana katika jambo hili.


Ndipo wanaume wote wa Yuda na Benyamini wakakusanyika katika muda wa siku tatu; ulikuwa mwezi wa tisa, siku ya ishirini ya mwezi; na watu wote wakaketi katika uwanja, mbele ya nyumba ya Mungu, wakitetemeka kwa sababu ya neno hilo, na kwa sababu ya mvua kubwa.


Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa umeme wa radi.


Maana yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka ukungu wake;


Je! Umeziingia ghala za theluji, Au umeziona ghala za mvua ya mawe,


Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani;


Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke, Upepo wa dhoruba utimizao neno lake.


Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.


basi waambie hao wanaoupaka ukuta chokaa isiyokorogwa vema, ya kwamba utaanguka; kutakuwa mvua ya kufurika; nanyi, enyi mvua ya mawe makubwa ya barafu, mtaanguka; na upepo wa dhoruba utaupasua.


Basi Bwana MUNGU asema hivi; Nitaupasua kwa upepo wa dhoruba, katika ghadhabu yangu; tena kutakuwa mvua ya barafu ya kufurika katika hasira yangu; na mawe makubwa ya barafu katika hasira ya kuukomesha.


Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA ndilo jina lake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo