Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 33:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 wapate kuachana na matendo yao mabaya, na kuvunjilia mbali kiburi chao.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 wapate kuachana na matendo yao mabaya, na kuvunjilia mbali kiburi chao.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 wapate kuachana na matendo yao mabaya, na kuvunjilia mbali kiburi chao.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 ili kumgeuza mtu kutoka kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,

Tazama sura Nakili




Yobu 33:17
16 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mke wa mtu.


Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse.


Walakini Hezekia hakuwa na shukrani kadiri alivyofadhiliwa; kwa kuwa moyo wake ulijawa na kiburi; kwa hiyo ikawako hasira juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu.


Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.


Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia mhuri mafundisho yao,


Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni, Na uhai wake usiangamie kwa upanga.


Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;


Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


BWANA wa majeshi ndiye aliyefanya shauri hili, ili kuharibu kiburi cha utukufu wote, na kuwaaibisha watu wa duniani wote pia.


Basi kwa ajili ya hayo, angalia, nitaiziba njia yako kwa miiba, nami nitafanya kitalu juu yake, asipate kuyaona mapito yake.


Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.


Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nilipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.


aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.


Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo