Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 3:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Mauzauza na giza nene yaikumbe, mawingu mazito yaifunike. Giza la mchana liitishe!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Mauzauza na giza nene yaikumbe, mawingu mazito yaifunike. Giza la mchana liitishe!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Mauzauza na giza nene yaikumbe, mawingu mazito yaifunike. Giza la mchana liitishe!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Giza na kivuli kikuu viikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.

Tazama sura Nakili




Yobu 3:5
25 Marejeleo ya Msalaba  

Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi, Na giza tupu liko katika kope zangu;


Maana asubuhi kwao wote ni kama giza tupu; Maana wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.


Binadamu hukomesha giza; Huyatafutatafuta hata katika maeneo ya mbali, Mawe ya madini katika giza, giza kuu.


Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.


Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.


Hapana hofu ya giza kuu, mahali wawezapo kujificha watendao udhalimu.


Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?


Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na minyororo,


Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akaivunja minyororo yao.


Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.


Japo ulituponda katika pango la mbwamwitu, Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.


Watu wale waliokwenda katika giza Wameona nuru kuu; Wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, Nuru imewaangaza.


Mtukuzeni BWANA, Mungu wenu, kabla hajaleta giza, na kabla miguu yenu haijakwaa juu ya milima yenye giza; na wakati mnapoitazamia nuru, kabla hajaigeuza kuwa kivuli cha mauti, na giza nene.


Wala hawakusema, Yuko wapi BWANA, aliyetutoa katika nchi ya Misri; akatuongoza jangwani, katika nchi ya ukame na mashimo, katika nchi ya kiu na ya kivuli cha mauti, katika nchi ambayo ndani yake hapiti mtu, wala haikukaliwa na watu?


Kwa ajili ya hayo nchi itaomboleza, na mbingu zitakuwa nyeusi; kwa sababu mimi nimeyanena haya, na kuyakusudia, wala sikujuta wala mimi sitarudi nyuma niyaache.


Kwa maana siku ile i karibu, siku ile ya BWANA i karibu, siku ya mawingu; itakuwa wakati wa maangamizi kwa mataifa.


Kama vile mchungaji atafutavyo kondoo wake, siku ile anapokuwa kati ya kondoo wake waliotawanyika; ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu; nami nitawaokoa katika mahali pote walipotawanyika, katika siku ya mawingu na giza.


siku ya giza na huzuni, siku ya mawingu na giza kuu. Kama mapambazuko yakitandazwa juu ya milima, hao ni wakuu, tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi.


mtafuteni yeye afanyaye Kilimia na Orioni, na kukigeuza kivuli cha mauti kuwa asubuhi, na kuufanya mchana kuwa giza usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA, ndilo jina lake;


Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upara katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.


Watu wale waliokaa katika giza Wameona mwanga mkuu, Nao waliokaa katika nchi na uvuli wa mauti Mwanga umewazukia.


Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.


Mkakaribia, mkasimama chini ya ule mlima; mlima ukawaka moto mpaka kati ya mbinguni, kwa giza na mawingu, na giza kuu.


Maana hamkufikia mlima uwezao kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo