Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 29:22 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

22 Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu; Matamko yangu yakadondoka juu yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza, maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza, maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza, maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.

Tazama sura Nakili




Yobu 29:22
14 Marejeleo ya Msalaba  

Sauti yao wakuu ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao.


Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua; Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika.


Bibi arusi, midomo yako yadondosha asali, Asali na maziwa viko chini ya ulimi wako; Na harufu ya mavazi yako Ni kama harufu ya Lebanoni.


ndivyo atakavyowastusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu.


Mwanadamu, uelekeze uso wako kusini, ukadondoze neno lako upande wa kusini, ukatabiri juu ya msitu wa uwanda wa Negebu,


Mwanadamu, uelekeze uso wako Yerusalemu, ukadondoze neno lako upande wa mahali patakatifu, ukatabiri juu ya nchi ya Israeli;


Efraimu aliponena, palikuwa na tetemeko; alijitukuza katika Israeli; Lakini alipokosa katika Baali, alikufa.


Basi, sasa lisikie neno la BWANA; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka;


Msitabiri, ndivyo watabirivyo; wasiyatabiri mambo haya; lawama hazikomi.


Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu.


Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu yeyote tangu siku ile kumwuliza neno tena.


Mafundisho yangu yatadondoka kama mvua, Maneno yangu yatatona-tona kama umande; Kama manyunyu juu ya majani mabichi; Kama matone ya mvua juu ya mimea.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo