Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 27:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Je! Mungu atakisikia kilio chake, Taabu zitakapomfikia?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Je, atakapokumbwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Je, atakapokumbwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Je, atakapokumbwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?

Tazama sura Nakili




Yobu 27:9
19 Marejeleo ya Msalaba  

Katika kuhukumiwa ataonekana hana haki, Na sala yake itadhaniwa kuwa ni dhambi.


Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa, Walimwita BWANA lakini hakuwajibu,


Nikawaponda kama mavumbi mbele ya upepo, Nikawatupa nje kama matope ya njiani.


Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia.


Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia.


Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.


Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo.


Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.


Basi, BWANA asema hivi, Tazama, nitaleta mabaya juu yao, ambayo hawataweza kuyakimbia; nao watanililia, lakini sitawasikiliza.


Wafungapo, mimi sitasikia kilio chao; na watoapo sadaka za kuteketezwa na sadaka ya unga, sitazitakabali; bali nitawaangamiza kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni.


Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitawaonea huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.


Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.


Ndipo watakapomwomba BWANA, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.


Ikawa kama wakati nilipowaita, wasitake kunisikiliza; basi, nao wataniita, wala sitasikiliza, asema BWANA wa majeshi.


Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;


Tunajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo.


Mkarudi mkalia mbele za BWANA; BWANA asiisikize sauti yenu, wala hakuelekeza masikio yake kwenu.


Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo