Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 27:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki; Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukweli mpaka kufa kwangu nasema sina hatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukweli mpaka kufa kwangu nasema sina hatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukweli mpaka kufa kwangu nasema sina hatia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.

Tazama sura Nakili




Yobu 27:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, ataniua; sina tumaini; Ila hata hivyo nitaithibitisha njia yangu mbele yake.


Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.


BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ijapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.


Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Mkufuru Mungu, ufe.


Nilijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.


(Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);


Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku chochote kimeshikamana na mikono yangu;


Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwenye haki machoni pake mwenyewe.


Ndipo zikawaka hasira za huyo Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, katika jamaa ya Ramu, juu ya Ayubu, kwa sababu alikuwa amejipa haki mwenyewe zaidi ya Mungu.


Tena hasira zake ziliwaka juu ya hao rafiki zake watatu kwa sababu hawakupata jawabu, lakini wamemhukumia Ayubu makosa.


Mimi ni safi, sina makosa; Sina hatia, wala hapana uovu ndani yangu;


Basi ikawa, baada ya BWANA kumwambia Ayubu maneno hayo, BWANA akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.


Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu; Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.


Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki; naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki; Hao wote wawili ni chukizo kwa BWANA.


Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.


Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nilishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu.


Pakiwa na mashindano kati ya watu, wakaenda maamuzini, na hao waamuzi wakawaamua; na wampe haki mwenye haki, na wamhukumie makosa yule mwovu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo