Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 23:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

10 Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunijaribu nitatoka humo safi kama dhahabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunijaribu nitatoka humo safi kama dhahabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunijaribu nitatoka humo safi kama dhahabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

Tazama sura Nakili




Yobu 23:10
32 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana nimemchagua ili awaamuru wanawe na vizazi vyake baada yake wadumishe njia ya BWANA, kwa kuwa wenye haki na kweli, ili BWANA naye akamtimizie Abrahamu ahadi zake.


Maana nimezishika njia za BWANA, Wala sikumwasi Mungu wangu.


Nakusihi, BWANA, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.


Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu; Wala hapana awezaye kuokoa kutoka kwa mkono wako?


Hapo waelekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.


Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kulia, hata nisimwone.


Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?


(Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);


Mimi ni safi, sina makosa; Sina hatia, wala hapana uovu ndani yangu;


Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu; Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.


Na kumwangalia kila asubuhi, Na kumjaribu kila dakika?


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


BWANA humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.


Umenijaribu moyo wangu, umenijia usiku, Umenichunguza usione neno; Nimenuia kinywa changu kisikose,


Kwa maana umetupima, Ee Mungu, Umetujaribu inavyojaribiwa fedha.


Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na fikira Ndiye Mungu aliye mwenye haki.


Kalibu ni kwa fedha, na tanuri kwa dhahabu; Bali BWANA huijaribu mioyo.


Lakini wewe, BWANA, wanijua; umeniona, umeujaribu moyo wangu, jinsi unavyokuelekea; uwakokote kama kondoo waendao kuchinjwa, ukawaweke tayari kwa siku ya kuchinjwa.


Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.


Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.


Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.


Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arubaini katika jangwa, ili akunyenyekeze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Kwa imani Abrahamu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;


Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji la uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.


ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo