Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 22:29 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

29 Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

29 Maana, Mungu huwaporomosha wenye majivuno, lakini huwaokoa wanyenyekevu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

29 Maana, Mungu huwaporomosha wenye majivuno, lakini huwaokoa wanyenyekevu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

29 Maana, Mungu huwaporomosha wenye majivuno, lakini huwaokoa wanyenyekevu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

29 Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

29 Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.

Tazama sura Nakili




Yobu 22:29
17 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye hawaondolei macho yake wenye haki; Lakini pamoja na wafalme huwaweka Katika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.


Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.


Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.


Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewainua.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo