Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 22:27 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

27 Utamwomba yeye naye atakusikia; Nawe utazitimiliza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

27 utamwomba naye atakusikiliza, nawe utazitimiza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

27 utamwomba naye atakusikiliza, nawe utazitimiza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

27 utamwomba naye atakusikiliza, nawe utazitimiza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

27 Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

27 Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.

Tazama sura Nakili




Yobu 22:27
22 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Yehoahazi akamsihi BWANA, BWANA akamsikiliza; kwa kuwa aliyaona mateso ya Israeli, jinsi mfalme wa Shamu alivyowatesa.


Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibariki kweli kweli, na kuipanua mipaka yangu, na mkono wako ukawa pamoja nami, nawe ungenilinda nisipatwe na maovu wala madhara! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.


Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba BWANA ndiye Mungu.


Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu, Na kumnyoshea mikono yako;


Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi, Na kumlingana Mungu nyakati zote?


Yeye humwomba Mungu, naye akamtakabalia; Hata auone uso wake kwa furaha; Naye humrejeshea mtu haki yake.


Hata wakafanya kilio cha maskini kumfikia, Naye akasikia kilio cha hao wateswao.


Ikiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.


Haleluya. Nampenda BWANA kwa kuwa anaisikiliza Sauti yangu na dua zangu.


Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA, Naam, mbele ya watu wake wote.


Ee Mungu, nadhiri zako ziko juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.


Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu. Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.


Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;


Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.


Ndipo utaita, na BWANA ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole, wala kunena maovu;


Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.


Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA.


Utakapoweka nadhiri kwa BWANA, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo