Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 19:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite amezitia giza njia zangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite amezitia giza njia zangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite amezitia giza njia zangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.

Tazama sura Nakili




Yobu 19:8
16 Marejeleo ya Msalaba  

Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso.


Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukigo?


Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya; Nami nilipongojea mwanga, likaja giza.


Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.


Njia ya waovu ni kama giza; Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.


Ni nani miongoni mwenu amchaye BWANA, aitiiye sauti ya mtumishi wake? Yeye aendaye katika giza, wala hana nuru, naye alitumainia jina la BWANA, na kumtegemea Mungu wake.


Kwa sababu hiyo hukumu ya haki iko mbali nasi, wala haki haitufikii; twatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu.


Mtukuzeni BWANA, Mungu wenu, kabla hajaleta giza, na kabla miguu yenu haijakwaa juu ya milima yenye giza; na wakati mnapoitazamia nuru, kabla hajaigeuza kuwa kivuli cha mauti, na giza nene.


Kwa ajili ya hayo njia yao itakuwa kwao kama mahali pa kuteleza gizani; watateremshwa na kuanguka hapo; kwa maana nitaleta uovu juu yao, naam, mwaka wa kujiliwa kwao, asema BWANA.


Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu.


Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Amenifunga kwa mnyororo mzito.


Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.


Basi kwa ajili ya hayo, angalia, nitaiziba njia yako kwa miiba, nami nitafanya kitalu juu yake, asipate kuyaona mapito yake.


Maana hakujua ya kuwa mimi ndiye niliyempa ngano, na divai, na mafuta, na kumwongezea fedha na dhahabu, walivyovitumia kwa ajili ya Baali.


Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.


Nao walipomlilia BWANA, akaweka giza kati yenu na Wamisri, akaileta bahari juu yao, akawafunikiza; nayo macho yenu yaliyaona mambo niliyoyatenda huko Misri; kisha mkakaa jangwani siku nyingi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo