Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 19:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Nioneeni huruma, nioneeni huruma enyi rafiki zangu; maana mkono wa Mungu umenifinya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Nioneeni huruma, nioneeni huruma enyi rafiki zangu; maana mkono wa Mungu umenifinya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Nioneeni huruma, nioneeni huruma enyi rafiki zangu; maana mkono wa Mungu umenifinya.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.

Tazama sura Nakili




Yobu 19:21
13 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.


Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.


Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.


Lakini sasa haya yamekufikia wewe, nawe wafa moyo; Yamekugusa, nawe wafadhaika.


Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki; Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.


Kwa kuwa mishale ya huyo Mwenyezi iko ndani yangu, Na roho yangu inainywa sumu yake; Vitisho vya Mungu vimejipanga juu yangu.


Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata.


Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote.


Basi, angalia, mkono wa Bwana uko juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazungukazunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.


Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.


Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.


Wakumbukeni hao waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao; na hao wanaodhulumiwa, kwa vile ninyi nanyi mlivyo katika mwili.


je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa BWANA umetoka juu yangu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo