Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 16:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

10 Wamenifumbulia vinywa vyao; Wamenipiga shavuni kwa kunitukana; Hukutana pamoja juu yangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Watu wananidhihaki na kunicheka; makundi kwa makundi hunizunguka, na kunipiga makofi mashavuni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Watu wananidhihaki na kunicheka; makundi kwa makundi hunizunguka, na kunipiga makofi mashavuni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Watu wananidhihaki na kunicheka; makundi kwa makundi hunizunguka, na kunipiga makofi mashavuni.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.

Tazama sura Nakili




Yobu 16:10
22 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo akakaribia Sedekia, mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Roho ya BWANA alitokaje kwangu ili aseme na wewe?


Ndipo akakaribia Sedekia mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Alitokaje kwangu Roho ya BWANA ili aseme na wewe?


Mungu amenitia kwa hao wapotovu, Na kunitupa mikononi mwao waovu.


Kwa mkono wangu wa kulia huinuka kundi; Huisukuma miguu yangu kando, Na kunipandishia njia zao za uharibifu.


Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma.


Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya moyo wangu.


BWANA, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.


Lakini nikijikwaa wanafurahi na kukusanyana, Walinikusanyikia watu ovyo nisiowajua, Wakanipapura bila kukoma.


Nao wananifumbulia vinywa vyao, Husema, Ewe! Ewe! Jicho letu limeona.


Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa waliniotea ili waniue.


Kwa pamoja wanaishambulia nafsi yake mwenye haki, Na kuihukumu damu isiyo na hatia.


Niliwatolea wapigao mgongo wangu, na wang'oao ndevu mashavu yangu; sikuficha uso wangu usipate fedheha na kutemewa mate.


Juu yako adui zako wote Wamepanua vinywa vyao; Huzomea, husaga meno yao, Husema, Tumemmeza; Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia; Tumeipata, tumeiona.


Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.


Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo.


Ndipo wakamtemea mate usoni, wakampiga ngumi; na wengine wakampiga makofi,


Basi aliposema hayo, mtumishi mmojawapo aliyesimama karibu alimpiga Yesu kofi akisema, Wamjibu hivi Kuhani Mkuu?


Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.


Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta,


Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo