Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 15:30 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

30 Hataondoka gizani; Ndimi za moto zitayakausha matawi yake, Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

30 Hatalikwepa giza la kifo. Ndimi za moto zitakausha chipukizi zake, maua yake yatapeperushwa na upepo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

30 Hatalikwepa giza la kifo. Ndimi za moto zitakausha chipukizi zake, maua yake yatapeperushwa na upepo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

30 Hatalikwepa giza la kifo. Ndimi za moto zitakausha chipukizi zake, maua yake yatapeperushwa na upepo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

30 Hatatoka gizani; mwali wa moto utanyausha machipukizi yake, nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

30 Hatatoka gizani; mwali wa moto utanyausha machipukizi yake, nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.

Tazama sura Nakili




Yobu 15:30
25 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani, Naye hungojewa na upanga;


Hutangatanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi? Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu naye;


Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa.


Chini, mizizi yake itakaushwa; Na juu, tawi lake litasinyaa.


Atakimbizwa kutoka mwangani hata gizani, Na kufukuzwa atoke duniani.


Giza lote linawekwa kwa ajili ya hazina zake; Moto ambao haukuvuviwa na mtu utamla; Utayateketeza yaliyosalia hemani mwake.


Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali, Na mabaki yao moto umeyateketeza.


Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu, Nao ungeyang'oa mavuno yangu yote.


Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.


Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, Hupapasa mchana vile vile kama usiku.


bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.


Maana Tofethi imewekwa tayari tokea zamani, naam, imewekwa tayari kwa mfalme huyo; ameifanya kubwa, inakwenda chini sana; tanuri yake ni moto na kuni nyingi; pumzi ya BWANA, kama mto wa kiberiti, huiwasha.


Kwa sababu hiyo nimewakatakata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu; na hukumu yangu itatokea kama mwanga.


Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Kisha atawaambia na wale walioko katika mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;


bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa.


ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.


Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili kwa upanga huo awapige mataifa. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo