Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 14:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 “Mtu ni mtoto tu wa mwanamke; huishi siku chache tena zilizojaa taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 “Mtu ni mtoto tu wa mwanamke; huishi siku chache tena zilizojaa taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 “Mtu ni mtoto tu wa mwanamke; huishi siku chache tena zilizojaa taabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.

Tazama sura Nakili




Yobu 14:1
20 Marejeleo ya Msalaba  

Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nilikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;


Yakobo akamjibu Farao, Siku za kuishi kwangu ni miaka mia moja na thelathini; siku za maisha yangu zimekuwa chache, tena za taabu, wala hazikufikia siku za maisha ya baba zangu katika siku za kuishi kwao.


Akamwambia baba yake, Kichwa changu! Kichwa changu! Naye akamwambia mtumishi wake, Mchukue kwa mama yake.


Je! Siku zangu si chache? Acha basi, Usinisumbue, nipate angaa kutulizwa moyo kidogo.


Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?


Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?


Tazama, hata mwezi hauangazi, Wala nyota si safi machoni pake;


Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate shida, Kama cheche za moto zirukavyo juu.


Je! Mtu hana huduma ngumu juu ya nchi? Na siku zake, je! Si kama siku za mwajiriwa?


Siku zangu hupita upesi kuliko chombo cha kufumia, Nazo zapita pasipokuwa na matumaini.


(Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;)


Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi; Zakimbia, wala hazioni mema.


Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri; Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako. Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.


Kweli, watu wote hupita kama kivuli; Wao hujisumbua bure tu; Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.


Tazama, nikazaliwa nikiwa na hatia; Mama yangu akanichukua mimba nikiwa na dhambi.


Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!


Basi, nikauchukia uhai; kwa sababu kazi inayotendeka chini ya jua ilikuwa mbaya kwangu; yaani, mambo yote ni ubatili na kufukuza upepo.


Kwa kuwa siku zake zote ni masikitiko, na kazi yake ni huzuni; naam, hata usiku moyoni mwake hamna raha. Hayo nayo ni ubatili.


Nilitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?


Lakini, nawaambieni, Hajatokea mtu katika wazawa wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; lakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo