Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 12:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

15 Tazama, yuayazuia maji, nayo yakatika; Tena, huyatuma, nayo yaipindua dunia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Akizuia mvua, twapata ukame; akiifungulia, nchi hupata mafuriko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Akizuia mvua, twapata ukame; akiifungulia, nchi hupata mafuriko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Akizuia mvua, twapata ukame; akiifungulia, nchi hupata mafuriko.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.

Tazama sura Nakili




Yobu 12:15
18 Marejeleo ya Msalaba  

Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila kiumbe umefika mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia maovu, basi nitawaangamiza pamoja na dunia.


Tazama, nitaleta gharika ya maji juu ya nchi, niharibu kila kitu chenye mwili na pumzi ya uhai, kisiwepo chini ya mbingu; kila kilichoko duniani kitakufa.


Katika mwaka wa mia sita wa maisha ya Nuhu, mwezi wa pili, siku ya kumi na saba ya mwezi, siku ile chemchemi zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu, madirisha ya mbinguni yakafunguka.


Na Mungu akamkumbuka Nuhu, na kila kilicho hai, na wanyama wote waliokuwamo pamoja naye katika safina; Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakapungua;


Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.


Ikawa, baada ya siku kupita, kile kijito kikakatika, kwa sababu mvua haikunyesha katika nchi.


Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, Na pumzi zao wanadamu wote.


Apate kuufanyia upepo uzito wake; Naam, anayapima maji kwa kipimo.


Je! Katika vitu vya ubatili vya mataifa, kiko kitu kiwezacho kuleta mvua? Je! Mbingu zaweza kutoa manyunyu? Je! Si wewe, Ee BWANA, Mungu wetu? Kwa sababu hiyo tutakungoja; kwa kuwa wewe umevifanya vitu hivi vyote.


mtafuteni yeye afanyaye Kilimia na Orioni, na kukigeuza kivuli cha mauti kuwa asubuhi, na kuufanya mchana kuwa giza usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA, ndilo jina lake;


Yeye huikemea bahari na kuikausha, pia huikausha mito yote; Bashani hulegea, na Karmeli; nalo ua la Lebanoni hulegea.


Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia katika nchi nzima;


hasira za BWANA zikawaka juu yenu, naye akafunga mbingu kusiwe na mvua, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo BWANA.


Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo