Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 12:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

10 Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, Na pumzi zao wanadamu wote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Uhai wa kila kiumbe hai umo mikononi mwake; kadhalika na pumzi ya uhai wa binadamu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Uhai wa kila kiumbe hai umo mikononi mwake; kadhalika na pumzi ya uhai wa binadamu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Uhai wa kila kiumbe hai umo mikononi mwake; kadhalika na pumzi ya uhai wa binadamu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.

Tazama sura Nakili




Yobu 12:10
17 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa kiumbe hai.


Tazama, nitaleta gharika ya maji juu ya nchi, niharibu kila kitu chenye mwili na pumzi ya uhai, kisiwepo chini ya mbingu; kila kilichoko duniani kitakufa.


(Kwa kuwa uhai wangu ungali mzima ndani yangu, Na Roho ya Mungu iko katika pua yangu;)


Maana tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida, Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?


Roho ya Mungu imeniumba, Na pumzi za Mwenyezi hunipa uhai.


Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao,


Waituma roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi.


Na kwa ajili ya hayo yote, nikatia moyo wangu katika kuyachunguza haya; ya kuwa wenye haki, na wenye hekima, pamoja na matendo yao yote, wamo mkononi mwa Mungu; iwe ni upendo au iwe ni chuki, mwanadamu hajui; mambo yote yawapita.


Mungu BWANA anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.


Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya.


Bali umejiinua juu ya Bwana wa mbingu; nao wamevileta vyombo vya nyumba yake mbele yako; na wewe, na wakuu wako, na wake zako, na masuria wako, mmevinywea; nawe umeisifu miungu ya fedha na ya dhahabu na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe; wasioona, wala kusikia, wala kujua neno lolote; na Mungu yule, ambaye pumzi yako i mkononi mwake, na njia zako zote ni zake, hukumtukuza.


Nao wakaanguka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?


Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.


wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu chochote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote.


Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazawa wake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo