Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 11:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

14 Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe, Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Kama una uovu, utupilie mbali. Usikubali ubaya uwemo nyumbani mwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Kama una uovu, utupilie mbali. Usikubali ubaya uwemo nyumbani mwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Kama una uovu, utupilie mbali. Usikubali ubaya uwemo nyumbani mwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako, wala usiuruhusu uovu ukae kwenye hema lako,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako wala usiuruhusu uovu ukae hemani mwako,

Tazama sura Nakili




Yobu 11:14
13 Marejeleo ya Msalaba  

Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, lakini yapasa uishinde.


Pamoja na hayo BWANA aliwashuhudia Israeli, na Yuda, kwa kinywa cha kila nabii, na cha kila mwonaji, akisema, Geukeni, na kuziacha njia zenu mbaya, mkazishike amri zangu na hukumu zangu, sawasawa na ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, nikawapelekea kwa kinywa cha manabii watumishi wangu.


Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa; Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.


Je! Uovu wako si mkuu? Wala maovu yako hayana mwisho.


Nisiyoyaona nifundishe wewe; Kama nimefanya uovu sitafanya tena?


Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au ni wapi hao waelekevu walikatiliwa mbali?


Ikiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.


Nitakuwa na mwenendo usio na hatia; Utakuja kwangu lini? Nitakwenda kwa unyofu wa moyo Ndani ya nyumba yangu.


Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.


Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.


Basi Samweli akawaambia nyumba yote ya Israeli, akasema, Ikiwa mnamrudia BWANA kwa mioyo yenu yote, basi, iondoleeni mbali miungu migeni, nayo Maashtorethi yatoke kwenu, mkamwelekezee BWANA mioyo yenu, mkamtumikie yeye peke yake; naye atawaokoa katika mikono ya Wafilisti.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo