Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 9:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

4 Jihadharini, kila mtu na jirani yake, wala msimtumaini ndugu awaye yote; maana kila ndugu atachongea, na kila jirani atakwenda huku na huko na kusingizia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Kila mmoja ajihadhari na jirani yake! Hata ndugu yeyote haaminiki, kila ndugu ni mdanganyifu, na kila jirani ni msengenyaji.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Kila mmoja ajihadhari na jirani yake! Hata ndugu yeyote haaminiki, kila ndugu ni mdanganyifu, na kila jirani ni msengenyaji.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Kila mmoja ajihadhari na jirani yake! Hata ndugu yeyote haaminiki, kila ndugu ni mdanganyifu, na kila jirani ni msengenyaji.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.

Tazama sura Nakili




Yeremia 9:4
28 Marejeleo ya Msalaba  

Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.


Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.


Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala kumtenda mwenziwe mabaya, Wala kumsengenya jirani yake.


Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.


Mtu amshuhudiaye jirani yake uongo Ni nyundo, na upanga, na mshale mkali.


Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.


Maana wao hula mkate wa uovu, Nao hunywa divai ya ujeuri.


Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.


Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.


katika kukosa na kumkana BWANA, na katika kugeuka tusimfuate Mungu wetu, tukinena udhalimu na uasi, na kukusudia maneno ya uongo na kuyatoa moyoni.


Kwa maana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao walioongozwa na watu hao wameangamia.


Kwa maana hata ndugu zako, na nyumba ya baba yako, wamekutenda mambo ya hila; naam, wamepiga kelele nyuma yako; usiwasadiki, wajapokuambia maneno mazuri.


Ni waasi kupita kiasi wote pia, waendao huku na huko wakisingizia, ni shaba na chuma hao, hutenda dhuluma wote pia.


Ulimi wao ni mshale ufishao; husema maneno ya hadaa; mtu mmoja husema maneno ya amani na mwenzake kwa kinywa chake, lakini moyoni mwake humwotea.


Wasingiziaji wamekuwamo ndani yako, ili kumwaga damu; na ndani yako wamekula juu ya milima; kati yako wamefanya uasherati.


Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.


Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu?


Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;


Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwaua.


Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawaua baadhi yenu.


Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosea katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo