Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 9:22 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

22 Nena, BWANA asema hivi, Mizoga ya watu itaanguka kama samadi juu ya mashamba, Na kama konzi ya ngano nyuma yake avunaye, wala hapana mtu atakayeikusanya.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Maiti za watu zimetapakaa kila mahali kama marundo ya mavi mashambani, kama masuke yaliyoachwa na mvunaji, wala hakuna atakayeyakusanya.’ Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Maiti za watu zimetapakaa kila mahali kama marundo ya mavi mashambani, kama masuke yaliyoachwa na mvunaji, wala hakuna atakayeyakusanya.’ Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Maiti za watu zimetapakaa kila mahali kama marundo ya mavi mashambani, kama masuke yaliyoachwa na mvunaji, wala hakuna atakayeyakusanya.’ Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Sema, “Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “ ‘Mizoga ya watu italala kama kinyesi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna atakayeikusanya.’ ”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Sema, “Hili ndilo asemalo bwana: “ ‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’ ”

Tazama sura Nakili




Yeremia 9:22
17 Marejeleo ya Msalaba  

Hezekia akawasikiliza, akawaonesha nyumba yote yenye vitu vyake vya thamani, fedha, na dhahabu, na manukato, na marhamu ya thamani, na nyumba yenye silaha zake, na vitu vyote vilivyoonekana katika hazina zake. Wala hapakuwa na kitu asichowaonesha Hezekia, katika nyumba yake, wala katika ufalme wake wote.


Ndipo akasema, Wameona nini nyumbani mwako? Hezekia akajibu, Vitu vyote vilivyomo nyumbani mwangu wameviona; hapana kitu nisichowaonesha katika hazina zangu.


Na mzoga wa Yezebeli utakuwa kama mavi juu ya uso wa mashamba, katika kiwanja cha Yezreeli; hata wasipate kusema, Huyu ni Yezebeli.


Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe; Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.


Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumlipa Mungu fidia kwa ajili ya maisha yake,


Ambao waliangamizwa Endori; Wakawa samadi juu ya nchi.


Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.


Usijitaabishe ili kupata utajiri; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.


Kwa sababu hiyo hasira ya BWANA imewaka juu ya watu wake, naye amenyosha mkono wake juu yao; akawapiga, navyo vilima vilitetemeka, na mizoga yao ilikuwa kama takataka katika njia kuu. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


watakufa kwa maradhi mabaya; hawataliliwa, wala hawatazikwa; watakuwa kama samadi juu ya uso wa nchi; nao wataangamizwa kwa upanga, na kwa njaa; na mizoga yao itakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.


Na waliouawa na BWANA siku ile watakuwapo, toka upande mmoja wa dunia hata upande wa pili; hawataliliwa, wala kukusanywa, wala kuzikwa; watakuwa samadi juu ya uso wa nchi.


Basi, kwa hiyo, BWANA asema hivi, Tazama, nitaweka makwazo mbele ya watu hawa, na baba na wana wao watajikwaa pamoja; jirani ya mtu na rafiki yake watapotea.


Na mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi; wala hapana mtu atakayewafukuza.


nao wataitawanya mbele ya jua, na mwezi, na jeshi lote la mbinguni, walivyovipenda, na kuvitumikia, na kuandamana navyo, na kuvitafuta, na kuviabudu haitakusanywa pamoja tena, wala kuzikwa; itakuwa ni samadi juu ya uso wa nchi.


Kisha atapita kwa kasi, kama upepo, atapita na kuwa ana hatia; yeye ambaye nguvu zake ni mungu wake.


Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda BWANA dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.


Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo