Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 8:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Mbona, basi, watu hawa wa Yerusalemu wamegeuka waende nyuma, wasikome kugeuka hivyo? Hushika udanganyifu sana, hukataa kurudi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Mbona basi, watu hawa wameacha njia iliyo sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikilia miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudia mimi!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Mbona basi, watu hawa wameacha njia iliyo sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikilia miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudia mimi!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Mbona basi, watu hawa wameacha njia iliyo sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikilia miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudia mimi!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Kwa nini basi watu hawa waliasi? Kwa nini Yerusalemu wanaasi kila mara? Wanang’ang’ania udanganyifu na wanakataa kurudi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanang’ang’ania udanganyifu na wanakataa kurudi.

Tazama sura Nakili




Yeremia 8:5
26 Marejeleo ya Msalaba  

Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.


bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga; maana kinywa cha BWANA kimenena haya.


wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;


Hula majivu; moyo uliodanganyika umempotosha, asiweze kuiokoa nafsi yake, wala kusema, Je! Sio uongo mkononi mwangu?


Ijapokuwa maovu yetu yanatushuhudia, lakini utende wewe kwa ajili ya jina lako, Ee BWANA, maana kurudi nyuma kwetu ni kwingi; tumekutenda dhambi.


Je! Mwanamwali aweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi mavazi yake? Lakini watu wangu wamenisahau mimi kwa muda wa siku zisizo na hesabu.


Je! Ataishika hasira yake hata milele? Ataishika hata mwisho? Tazama, umesema hivyo, bali umetenda mambo mabaya, umefuata njia yako mwenyewe.


Kama tundu lijaavyo ndege, kadhalika nyumba zao zimejaa hila; kwa hiyo wamekuwa wakuu, wamepata mali.


Ee BWANA, macho yako je! Hayaangalii uaminifu? Umewapiga, lakini hawakuhuzunika; umewakomesha, lakini wamekataa kurudiwa wamefanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba wamekataa kurudi.


Basi, kwa hiyo, simba atokaye mwituni atawaua, mbwamwitu wa jioni atawateka, chui ataivizia miji yao, kila mtu atokaye humo atararuliwa vipande vipande; kwa sababu makosa yao ni mengi, na kurudi nyuma kwao kumezidi.


Nami niliweka walinzi juu yenu, wakisema, Isikilizeni sauti ya tarumbeta; lakini walisema, Hatutaki kusikiliza.


Sikia, Ee nchi; tazama, nitaleta mabaya juu ya watu hawa, naam, matunda ya mawazo yao, kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu; tena kwa habari ya sheria yangu, wameikataa.


Makao yako ya katikati ya hadaa; kwa hadaa wanakataa kunijua mimi, asema BWANA.


Naam, Israeli wote wameivunja sheria yako, kwa kugeuka upande, wasiisikilize sauti yako; basi kwa hiyo laana imemwagwa juu yetu, na kiapo kile kilioandikwa katika Sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu; kwa sababu tumemtenda dhambi.


Hatarudi tena nchi ya Misri; bali huyo Mwashuri atakuwa mfalme wake; kwa sababu walikataa kurejea.


Na watu wangu wamejipinda kuniacha; ingawa wawaita kwenda kwake Aliye Juu, hapana hata mmoja atakayemtukuza.


Na sasa wanazidi kufanya dhambi, nao wamejifanyia sanamu kwa fedha yao, naam, sanamu kwa kadiri ya akili zao; zote pia ni kazi ya mafundi; nao huzitaja hivi, Wanaume watoao dhabihu na wazibusu ndama.


Kwa maana Israeli ametenda kwa ukaidi, kama ndama mkaidi; sasa je! BWANA atawalisha kama mwana-kondoo katika mahali penye malisho mazuri.


Lakini hao walikataa kusikiliza, wakageuza bega lao, wakaziba masikio yao ili wasisikie.


Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima.


jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;


Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni;


Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo