Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 6:28 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

28 Ni waasi kupita kiasi wote pia, waendao huku na huko wakisingizia, ni shaba na chuma hao, hutenda dhuluma wote pia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

28 Wote ni waasi wakaidi, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, wagumu kama shaba nyeusi au chuma; wote hutenda kwa ufisadi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

28 Wote ni waasi wakaidi, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, wagumu kama shaba nyeusi au chuma; wote hutenda kwa ufisadi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

28 Wote ni waasi wakaidi, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, wagumu kama shaba nyeusi au chuma; wote hutenda kwa ufisadi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.

Tazama sura Nakili




Yeremia 6:28
19 Marejeleo ya Msalaba  

Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema.


Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.


Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.


Mwelekeeni yeye mliyemwasi sana, enyi wana wa Israeli.


Hapo ndipo waliposema, Njooni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njooni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yoyote.


Maana nimesikia shutuma za watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.


Lakini watu hawa wana moyo wa kuasi na ukaidi; wameasi, wamekwenda zao.


Watu watawaita taka za fedha, kwa sababu BWANA amewakataa.


Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya BWANA, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali na vinywa vyao.


Huupinda ulimi wao, kana kwamba ni upinde, ili kusema uongo; nao wamepata nguvu katika nchi, lakini si katika uaminifu; maana huendelea toka ubaya hata ubaya, wala hawanijui mimi, asema BWANA.


Jihadharini, kila mtu na jirani yake, wala msimtumaini ndugu awaye yote; maana kila ndugu atachongea, na kila jirani atakwenda huku na huko na kusingizia.


Nawe utawaambia maneno yangu, iwe watasikia au hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.


Katika uchafu wako mna uasherati, kwa maana nimekusafisha, ila wewe hukusafika; hutasafishwa tena uchafu wako ukutoke, hadi nitakapokuwa nimeituliza hasira yangu kwako.


Na kama hilo pigo likirudi tena, na kutokea ndani ya nyumba, baada ya yeye kuyatoa hayo mawe, na baada ya kuikwangua nyumba, na baada ya kupakwa chokaa,


Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.


Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja, na wakati ukaja wa kuhukumiwa waliokufa, na wa kuwapa thawabu yao watumishi wako manabii na watakatifu, na hao walichao jina lako, wadogo kwa wakubwa, na wa kuwaharibu hao waiharibuo nchi.


kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na haki; maana amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na kuipatiliza damu ya watumwa wake mkononi mwake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo