Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 6:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

10 Niseme na nani na kushuhudia, wapate kusikia? Tazama, sikio lao halikutahiriwa, wala hawawezi kusikiliza; tazama, neno la BWANA limekuwa matukano kwao; hawalifurahii.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Nitaongea na nani nipate kumwonya, ili wapate kunisikia? Tazama, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Kwao neno lako, ee Mwenyezi-Mungu, limekuwa jambo la dhihaka, hawalifurahii hata kidogo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Nitaongea na nani nipate kumwonya, ili wapate kunisikia? Tazama, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Kwao neno lako, ee Mwenyezi-Mungu, limekuwa jambo la dhihaka, hawalifurahii hata kidogo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Nitaongea na nani nipate kumwonya, ili wapate kunisikia? Tazama, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Kwao neno lako, ee Mwenyezi-Mungu, limekuwa jambo la dhihaka, hawalifurahii hata kidogo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Mwenyezi Mungu ni chukizo kwao, hawalifurahii.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.

Tazama sura Nakili




Yeremia 6:10
40 Marejeleo ya Msalaba  

Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.


Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.


Ee BWANA, nimeutamani wokovu wako, Na sheria yako ndiyo furaha yangu.


Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.


Uniendeshe katika mapito ya amri zako, Kwa maana nimependezwa nayo.


Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Lakini mimi nimeifurahia sheria yako.


Rehema zako zinijie nipate kuishi, Maana sheria yako ni furaha yangu.


Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.


Musa akanena mbele za BWANA, akasema, Tazama, hao wana wa Israeli hawakunisikiza mimi; basi huyo Farao atanisikizaje, mimi niliye na midomo isiyo tohara?


Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake yako wazi, lakini hasikii.


Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?


BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nenda ukawaambie wana wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, Je! Hamtaki kupokea mafundisho, myasikilize maneno yangu? Asema BWANA.


Jitahirini kwa BWANA, mkayaondoe magovi ya mioyo yenu, enyi watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu; ghadhabu yangu isije ikatoka kama moto, ikawaka hata mtu asiweze kuizima, kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.


Sikilizeni neno hili, enyi watu wajinga msio na ufahamu; mlio na macho ila hamuoni; mlio na masikio ila hamsikii.


Na sasa, kwa sababu mmezifanya kazi hizi zote asema BWANA, nami nikasema nanyi, nikiamka mapema na kunena, lakini hamkusikia; nami nikawaita wala hamkuniitikia;


Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao.


Misri, na Yuda, na Edomu, na wana wa Amoni, na Moabu, na wote wenye kunyoa denge, wakaao nyikani; maana mataifa hayo yote hawana tohara, wala nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa mioyo yao.


Bali nyumba ya Israeli hawatakusikiliza wewe; kwa kuwa hawanisikilizi mimi; maana nyumba yote ya Israeli wana vipaji vigumu, na mioyo yenye ukaidi.


akiona upanga unakuja juu ya nchi hiyo, na kupiga tarumbeta na kuwaonya watu;


Lakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako.


Ndipo Amazia, kuhani wa Betheli, akapeleka habari kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosi amefanya fitina juu yako kati ya nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote.


Na alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazawa wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?


Mtu mmoja katika wanasheria akajibu, akamwambia, Mwalimu, kwa kusema hayo umetushutumu sisi nasi.


Nao waandishi na wakuu wa makuhani walitaka kumkamata saa iyo hiyo, wakawaogopa watu, maana walitambua ya kwamba mfano huu amewanenea wao.


Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu.


Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?


Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.


Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona kitendo cha kuuawa kwake kuwa sawa.


Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani,


lakini BWANA hakuwapa moyo wa kujua, wala macho ya kuona, wala masikio ya kusikia, hata leo hivi.


ambaye sisi tunamhubiri habari zake tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, tupate kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo.


Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajikusanyia waalimu wengi, watakaowaambia yale tu masikio yao yanataka kusikia;


Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuiokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo