Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 50:35 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

35 Upanga uko juu ya Wakaldayo, asema BWANA, na juu yao wakaao Babeli, na juu ya wakuu wake, na juu ya watu wake wenye hekima.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

35 “Kifo kwa Wakaldayo, kwa wakazi wa Babuloni na maofisa na wenye hekima wake!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

35 “Kifo kwa Wakaldayo, kwa wakazi wa Babuloni na maofisa na wenye hekima wake!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

35 “Kifo kwa Wakaldayo, kwa wakazi wa Babuloni na maofisa na wenye hekima wake!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Mwenyezi Mungu, “dhidi ya wale wanaoishi Babeli, na dhidi ya maafisa wake na wenye busara!

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!

Tazama sura Nakili




Yeremia 50:35
22 Marejeleo ya Msalaba  

kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa.


Nimemwinua mtu toka kaskazini, naye amekuja; toka maawio ya jua amekuja anitajaye jina langu; naye atawakanyaga watawala kama akanyagaye matope, na kama mfinyanzi apondaye udongo.


Nizitanguaye ishara za waongo, na kuwatia waganga wazimu; niwarudishaye nyuma wenye hekima, na kuyageuza maarifa yao kuwa ujinga;


Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kulia, ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza nguvu za wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa.


Kwa maana BWANA atatoa hukumu kwa watu wote kwa moto, na kwa upanga wake, nao watakaouawa na BWANA watakuwa wengi.


Ni nani asiyekucha wewe, Ee mfalme wa mataifa? Maana hii ni sifa yako wewe; kwa kuwa miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa, na katika hali yao ya enzi yote pia, hapana hata mmoja kama wewe.


Ee upanga wa BWANA, Siku ngapi zitapita kabla hujatulia? Ujitie katika ala yako; Pumzika, utulie.


Wachinjeni mafahali wake wote; Na wateremkie machinjoni; Ole wao! Maana siku yao imewadia, Wakati wa kujiliwa kwao.


Kwa sababu hiyo vijana wake wataanguka katika njia zake kuu, na watu wake wa vita, wote pia, watanyamazishwa katika siku hiyo, asema BWANA.


Wakiingiwa na ukali, nitawafanyia karamu yao, nami nitawalevya, wapate kufurahi, na kulala usingizi wa milele, wasiamke tena, asema BWANA.


Basi angalia, siku zitakuja, ambazo katika siku hizo, nitafanya hukumu juu ya sanamu za Babeli, na nchi yake yote itatahayarika; na watu wake wote waliouawa wataanguka katikati yake.


Nami nitawalevya wakuu wake, na watu wake wenye hekima, watawala wake, na makamanda wake, na mashujaa wake; nao watalala usingizi wa milele, wasiamke, asema Mfalme, BWANA wa majeshi, ambaye jina lake ni BWANA.


Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la BWANA, wana akili gani ndani yao?


Ndipo neno la BWANA likanijia, kusema,


Usiku huo huo Belshaza, mfalme wa Wakaldayo, akauawa.


Na upanga utaiangukia miji yake, utayaharibu makomeo yake na kuyala, kwa sababu ya mashauri yao wenyewe.


Nami nitaleta upanga juu yenu, utakaopatiliza kisasi cha hilo agano; nanyi mtakutanishwa ndani ya miji yenu; nami nitaleta tauni kati yenu; nanyi mtatiwa mikononi mwa adui.


Ole wake mchungaji asiyefaa, aliachaye kundi! Upanga utakuwa juu ya mkono wake, na juu ya jicho lake la kulia; mkono wake utakuwa umekauka kabisa, na jicho lake la kulia litakuwa limepofuka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo