Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 50:32 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

32 Na mwenye kiburi atajikwaa, na kuanguka, wala hapana atakayemwinua; nami nitawasha moto katika miji yake, nao utawala wote wamzungukao pande zote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

32 Mwenye kiburi atajikwaa na kuanguka, wala hapatakuwa na mtu wa kumwinua. Nitawasha moto katika miji yake, nao utateketeza kila kitu kandokando yake.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

32 Mwenye kiburi atajikwaa na kuanguka, wala hapatakuwa na mtu wa kumwinua. Nitawasha moto katika miji yake, nao utateketeza kila kitu kandokando yake.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

32 Mwenye kiburi atajikwaa na kuanguka, wala hapatakuwa na mtu wa kumwinua. Nitawasha moto katika miji yake, nao utateketeza kila kitu kandokando yake.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

Tazama sura Nakili




Yeremia 50:32
22 Marejeleo ya Msalaba  

Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.


Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.


Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Nami nitawaadhibu kwa kadiri ya matendo yenu, asema BWANA; nami nitawasha moto katika msitu wake, nao utateketeza vitu vyote viuzungukavyo.


Nami nitawasha moto katika ukuta wa Dameski, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi.


Wala hawatatwaa kwako jiwe moja liwe la pembeni, wala jiwe moja liwe msingi; bali wewe utakuwa ukiwa daima, asema BWANA.


nawe utasema, Hivyo ndivyo utakavyozama Babeli, wala hautazuka tena, kwa sababu ya mabaya yote nitakayoleta juu yake; nao watachoka. Maneno ya Yeremia yamefika hata hapa.


Lakini moyo wake ulipoinuliwa, na roho yake ilipokuwa ngumu akatenda kwa kiburi, alishushwa katika kiti chake cha enzi, nao wakamwondolea utukufu wake.


lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Tiro, nao utayateketeza majumba yake.


lakini nitatuma moto juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra.


lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na tufani katika siku ya chamchela;


lakini nitatuma moto uingie katika nyumba ya Hazaeli, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi.


lakini nitatuma moto juu ya ukuta wa Gaza, nao utayateketeza majumba yake.


lakini nitatuma moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta;


lakini nitatuma moto juu ya Yuda, nao utayateketeza majumba ya Yerusalemu. Hukumu kwa Israeli.


Bikira wa Israeli ameanguka; hatainuka tena; Ameangushwa katika nchi yake; hakuna mtu wa kumwinua.


Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu, Unateketea hata chini ya kuzimu, Unakula dunia pamoja na mazao yake, Unaunguza misingi ya milima.


Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo